Yanga, Azam Kucheza Nyumbani FA Cup
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeiweka hadharani ratiba ya Raundi ya Nne ya Kombe la FA ambapo mechi zake zitachezwa kati ya Januari 25 na 28, mwaka huu.
Katika ratiba hiyo inayojumuisha timu 32, Yanga na Azam FC zitacheza mechi zao nyumbani sambamba na mabingwa watetezi, Mtibwa Sugar.
Ratiba kamili ya michuano hiyo ipo hivi; Rhino Rangers vs Stand United, KMC vs Pan African, Kagera vs Mbeya Kwanza, Polisi Tanzania vs Lipuli, Yanga vs Biashara, Kitayosce vs Coastal Union, Azam vs Pamba na Singida vs JKT Tanzania.
Mtibwa vs Majimaji, Mashujaa vs Mbeya City, African Lyon vs Friend Rangers, Mighty Elephant vs Namungo, Alliance vs La Familia, Dodoma vs Transit Camp, Cosmopolitan vs Dar City na Reha vs Boma.
Fainali ya mwaka huu imepangwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Ilulu uliopo Lindi ambapo bingwa ataiwakilisha Tanzania Bara kwenye Kombe la Shirikisho Afrika msimu ujao.
Comments are closed.