The House of Favourite Newspapers

SERENGETI LITE WAMEIBUA MENGI SOKA LA WANAWAKE

KINACHOONEKANA kwenye Ligi Kuu ya Wanawake msimu huu maarufu kama ‘Serengeti Lite Womens Premier League’ kinafurahisha. Kuna mam­bo mengi ambayo wadau hawaku­tarajia lakini yanatokea.

 

Kwanza ushindani ume­kuwa mkubwa viwanjani, ligi im­ekuwa na mvuto, mastaa wengi wapya wameibuliwa na vilevile mashabiki wengi wanajitokeza viwanjani haswa Dar es Salaam.

Udhamini wa Serengeti Lite kwenye ligi hiyo ku­mechangia kuongeza mvuto kwani timu zimewezeshwa zikafanya mambo ambayo mashabiki walikua wakiyata­mani.

 

Ligi hiyo imekuwa na mvuto kiasi kwamba hata baadhi ya timu zimesajili mastaa kutoka nje ya nchi ili kufanya vizuri zaidi.

Ligi hii inaundwa na timu 12 kuto­ka maeneo tofauti. JKT Queens na Mlandizi Queens zinatokea Pwani, Simba Queens, Yanga Princess na EverGreen Queens zinatokea Dar.

 

Sisterz FC ya Kigoma, Panama FC (Iringa), Alliance Girls na Marsh Academy za Mwan­za, Tanzanite SC (Arusha), Baobab Queens (Dodoma) na Mapinduzi Queens kuto­ka Njombe.

 

Kila mkoa hamasa im­ekuwa ni kubwa zaidi ya msimu uliopita jambo ambalo linaonyesha uwepo wa mdhamini umechangia. Maafande wa JKT Queens ndiyo mabingwa watetezi wa ligi hiyo wak­itwaa ubingwa huo msimu uliopita pasipo kupoteza mchezo wowote.

 

Nyota wao ni Fatuma Mustapha. Aliibuka mfungaji bora msimu uli­opita baada ya kutumbukia kambani mabao 18. Msimu huu pia ameanza na moto na ana mabao 17 kwenye michezo sita pekee mpaka sasa.

 

Kabla ya mechi za jana jioni, timu zote zilicheza mara sita huku JKT Queens ikiwa kileleni baada ya kuvuna alama 18 kuto­kana na kushinda michezo yote sita.

 

Lakini macho na masikio ya wapenzi wengi wa soka yapo kwa timu mbili ambazo ni watani wa jadi, Simba Queens na Yanga Princess.

 

Januari 13, mwaka huu zilicheza jijini Dar na Yanga akajikuta aki­ambulia kipigo cha mabao 7-0 licha ya kuonyesha ush­indani.

 

Nikiwa shuhu­da wa mchezo ule, niliona Sim­ba walistahili kushinda kwa zaidi ya mabao hayo kwa sababu uimara wa kikosi chao ambacho in­aonekana uongozi umeamua kuwekeza.

Safu ya ushambuliaji ya Simba Queens ikion­gozwa na Mwanahamisi Omary ‘Gaucho’ ni imara na imekuwa ikich­achafya kwenye ligi hiyo.

Kwenye mechi ya watani wa jadi, fowadi ya Simba ilitengeneza nafasi nyingi ambazo huenda zingezaa ma­bao mengi zaidi lakini na suala la ku­kosa uzoefu nalo likachangia.

 

Gaucho aliifungia timu yake mabao manne huku akikosa na­fasi zingine nne ambazo kama an­gekuwa mtulivu zaidi basi angeweza kuweka mpira kimiani katika nafasi zote alizopata zaidi ya saba.

 

Yanga licha ya kwamba im­eonyesha uhai laki­ni bado inahi­taji kuwekeza kwenye soka la wanawake. W a m e k o s a wachezaji ambao wana uwezo binafsi wa kupambana na kutafuta ma­tokeo ya ushindi na inaonekana hawakufanya maandalizi mazuri.

Simba Queens wanaonekana kui­marika zaidi kadiri siku zinavyozidi kwenda tofauti na Yanga Princess ambayo ni dhahiri inaonekana ina­kumbana na changamoto kadhaa za nje ya uwanja.

 

Simba imewaleta nyota wa ki­mataifa kutoka Burundi, Johelle Bukuru na Asha Djafar ambao wam­eonyesha kiwango kizuri kinachow­apa changamoto wachezaji wazawa.

 

Kwa hali ilivyo hivi sasa kama Simba wataendelea kukua kwa kasi yao hii inayoonekana basi bila shaka msimu ujao wanaweza kutwaa taji hili.

 

Yanga wanahitaji umakini zaidi kwenye usajili ili kufika pale wal­ipo wenzao kwa sababu timu yao inahitaji maboresho machache ili iwe na uwezo wa kupambana kwenye kiwango cha juu zaidi katika mashindano hayo na mengine.

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO

Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.