The House of Favourite Newspapers

KOULIBALY JEMBE LENYE SIFA ZA KUIBEBA MAN UNITED

Beki wa Napoli, Kalidou Koulibaly

MSIMU uliopita kabla ya Liverpool kumsajili beki wa kati, Virgil van Dijk, Liver­pool ilikuwa inatisha kwa kuwa na safu kali ya ush­ambuliaji. Hata hivyo, waka­ti Liverpool ikitupia mabao mengi kutokana na kuwa wafungaji hatari Mohamed Salah, Roberto Firmino na Sadio Mane lakini beki yao ilikuwa inapwaya.

 

Kocha wa Liverpool, Jur­gen Klopp alifahamu tatizo lake akaamua kumwaga kitita cha pauni milioni 75 na kum­sajili Van Dijk, Januari mwaka jana.

Mwanzoni mwa msimu huu wa 2018/19, Liverpool ika­jitosa kumsajili kipa Alisson na tayari Liverpool inafaidi matunda yake.

Liverpool ipo kwenye na­fasi za juu za Ligi Kuu Eng­land ikipewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa msimu huu.

 

Hali kama hivyo inawaka­bili Manchester United kwani inatisha kwa sasa chini ya kocha wao wa muda, Ole Gunnar Solskjaer, ambapo imeshinda mechi sita mfu­lulizo tena kwa idadi kubwa ya mabao.

Tatizo kubwa sasa kwa Manchester United liko kwenye beki ingawa bahati nzuri ina kipa mzuri, David De Gea.

United imepachika mabao 44 katika mechi 22 za Ligi Kuu England msimu huu, am­bapo imezidiwa mabao 15 na Manchester City. Klabu hiyo haina tatizo katika kufunga mabao lakini changamoto ya United ipo kwenye beki kwani i m ­eruhusu mabao 32.

 

Man United inahitaji sasa beki imara wa kati, mwenye nguvu, mpiganaji na mwenye uwezo wa kuongoza timu.

Klabu hiyo inasemekana inataka kumsajili beki wa Napoli, Kalidou Koulibaly, ambaye kwa sifa alizonazo ndio mtu ataifaa Manchester United kurudisha enzi wakati ilipokuwa na ukuta mgumu ulioundwa na mabeki wazuri kama Rio Ferdinand, Neman­ja Vidic na Jaap Stam.

 

Sifa za Koulibaly, ambaye anahesabiwa kama miongoni mwa mabeki bora duniani na anatesa kwenye Serie A ni hizi:

HAPITIKI KIRAHISI

Sifa ya kwanza ya Kouli­baly ni kutopitika kwake kira­hisi kutokana na uwezo wake mkubwa wa kusoma wapin­zani.

Koulibaly mwenye urefu w a mita195, ana uwezo mkubwa wa kupokonya mipira kutoka kwa mastraika wa timu pin­zani.

 

Pia ni mzuri wa mipira ya juu ya vichwa, ambapo ana­tazamiwa kutengeneza safu nzuri ya ulinzi ya United aki­shirikiana na Victor Lindelof.

Lindelof aliwahi kukaririwa siku za nyuma akidai anataka beki mwenzake mwenye nguvu kwa ajili ya kuche­za naye.

Sasa akiletewa Kouli­baly ina maana ndoto ya Lindelof itakuwa imetimizwa na sasa watatengeneza safu nzuri ya ulinzi itakayoweza ku­kabiliana na washam­buliaji wakali dun­iani.

 

Kouli­baly ni beki mzuri kwa kuwa ni mt u l i v u na ana uwezo mkubwawa kusoma timu pin­zani kiasi ambacho atasaidia mas­traika kuwa na kazi ya kupachika mabao.

 

BEKI MWENYE MBIO

Ni shughuli pevu kwa beki yeyo­te kuchezea timu inayocheza soka la kushambulia kama Manchester United.

Hata hivyo, bado kwa timu inayocheza soka la kushambulia lazima iwe na beki imara.

Pamoja na United kuwa na wachezaji wazuri wa kiungo lakini bado inahitaji beki.

 

Ni hasa pale inapo­tokea timu inasham­buliwa kwa `counter attack’ ambapo ndio anahitajika beki kwenye mbio wa kuzima masham­bulizi.

 

Koulibaly anasifika kutoka­na na kuwa na mbio, ambapo atasaidia kwa kiasi kikubwa kwa Manchester United ku­peleka mashambulizi kwa timu pinzani bila ya kuwa na wasiwasi kwani watakuwa na beki imara.

 

KUONGOZA TIMU

Manchester United haina kion­gozi kwenye safu yake ya ulinzi kama alivyo Van Dijk kwenye timu ya Liverpool.

Van Dijk anafanya kazi nzuri kama kocha akiwa uwanjani kuto­kana na mara nyingi kuwahimiza wenzake kuhakikisha wanajipanga na kuwa katika nafasi muafaka kila mara.

Koulibaly amekuwa anafanya kazi kama kiongozi wa timu pale Napoli.

 

Beki huyu kwanza mwenyewe hujiamini na pia huhakikisha hu­wapanga wenzake ili kuondo­sha hatari zote zinazoelekezwa kwenye goli lao.

 

Koulibaly mara zote hucheza kwa kujituma na mara nyingi hu­wasukuma wenzake kuhakikisha wanapata matokeo mazuri pale wanapokuwa uwanjani.

Beki huyo alikuwa na mchango mkubwa katika kuisaidia Napoli kufuku­zana vikali na Juventus kwenye Serie A msimu uliopita wa 2017/18 in­gawa hawakufanikiwa kutwaa ubingwa.

Kama Manches­ter United itafanikiwa kumpata Koulibaly basi atasaidia kwa kiasi kikubwa ku­maliza tatizo lao la kup­waya beki.

LONDON, England

BAUNSA AMFANYIA UBABE MKE WA MTU, MUME AWA MPOLE

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO

Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.