The House of Favourite Newspapers

MENINAH KUMBE AMEONA UZURI SIYO DILI

IKIWA baadhi ya wanawake wengi wanaamini kuwa ukijaaliwa uzuri wa sura na umbo ndiyo umemaliza kila kitu, kwa mwanamuziki na msanii wa filamu za Kibongo, Meninah Atik, uzuri kwake siyo dili na badala yake kikubwa ni kufanya kazi.

 

Akistorisha na Shusha Pumzi, Meninah alisema ameamua kupiga kazi bila kuchagua ndiyo maana akipata kazi ya U-MC, muziki na uigizaji anapiga kotekote ilimradi tu mkwanja uingie mfukoni.

 

“Kuna wakati ninajisahau kama mimi
ni mrembo kwa jinsi tu ninavyosaka mkwanja ili niweze kujenga maisha na kutimiza ndoto ambazo nimejiwekea,” alisema Menina

STORI: Imelda Mtema

Comments are closed.