The House of Favourite Newspapers

Sheikh Kishki Atembelea Ofisi za Global Group

Sheikh Nurdeen Kishki.

MSIMAMIZI Mkuu wa Taasisi ya Al Hikma Foundation, Sheikh Nurdeen Kishki,    leo Alhamisi Oktoba 17, 2019M  amefanya ziara katika ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori  Dar es salaam,  kwa lengo la kujionea utendaji kazi wa Idara mbalimbali.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Global Radio baada ya ziara hiyo, Sheikh Kishki amesema kutokana na kazi zinazozalishwa na vituo pendwa vya Global Group amevutiwa kujifunza vinavyofanya kazi.

Aidha amekumbushia umuhimu wa kuzingatia maadili katika jamii na kuepuka vitendo viovu vikiwemo vya matumizi mabaya mitandao.

Pia ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi umuhimu wa kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura na kuwachagua viongozi wanaostahili kuwaongoza.

Sheikh Kishki akisalimiana na mtangazaji wa kipindi cha Mid-Morning Fresh, Darboy.
Meneja wa Global Publishers, Abdallah Mrisho akiwa na nje Sheikh Kishki nje ya studio ya Global Radio baada ya mahojiano.
Sheikh Kishki akiwaombea dua wafanyakazi wa Global Group (hawapo pichani).
…Akiongea na Mrisho. 
…Akimwombea dua Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo (katikati).
…Akiwa na Meneja wa Global Radio, Bori Mbaraka (kushoto) na Kiongozi wa Global TV Online , Abdalla Ng’anzi (kulia)

Comments are closed.