The House of Favourite Newspapers

TRA Yakusanya Trilioni 1.04 Februari

0
1
Katika Kipindi cha miezi nane  kuanzia  Julai 2015 hadi Februari mwaka huu, Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imekusanya jumla ya Sh  Trilioni 8,569,854.40  ikilinganishwa na lengo la kukusanya Sh trilioni 8,685,991.52 ambayo ni sawa na asilimia 99 ya makusanyo yote.
Hayo yamesemwa leo na Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo, Alphayo Kidata wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu  mwenendo wa ukusanyaji wa mapato, matumizi ya mashine za EFDs, kusitisha kwa bei elekezi na usajili wa vyombo vya moto.
Amesema lengo la Mamkala hiyo ni kukusanya Trilioni 12.3 hadi ifikapo Juni mwaka huu na kwamba asilimia moja iliyobakia katika kukamilisha asilimia 100 ya ukusanyaji wa mapato kati ya Julai mwaka jana  hadi Juni mwaka huu,  itakamilika ndani ya miezi nne iliyosalia ambayo itaisha Juni mwaka huu.
Amesema pia kwa mwezi Februai pekee, Mamlaka hiyo imefanikiwa kukusanya mapato ya kiasi cha Sh Trilioni 1,040,540.20 kwa upande wa Tanzania  Bara na Zanziba ambayo kiasi hicho ni sawa na asilimia 101.18 ya lengo la ukusanyaji ambayo ilikuwa ni Sh  Trilioni  1,028,379.40 kwa mwezi.
Amesema kuongezeka kwa mapato haya kunatokana na kudhibiti kwa mianya ya ukwepaji wa kodi na kuweka mazingira rafiki kwa mlipa kodi, kurekebishwa kwa misamaha ya kodi ambayo ilikuwa inachangia upotevu wa mapato, kuongezeka kwa watumiaji wa mashine za EFDs pamoja kudhibiti eneo la forodha ambalo lilikuwa linasababisha upotevu wa mapato ya TRA.
Maeneo yaliyochangia kuongezeka kwa mapato hayo:  
“Maeneo ambayo yamechangia kuongezeka wa mapato haya ni kuimarishwa kwa bandari yetu kwa kuziba mianya ya ukwepaji kodi , kurekebishwa kwa misamaha ya kodi ambayo hapo awali ilikuwa inachangia upotevu wa ukusanyaji wa mapato, kuongezeka kwa matumizi ya utumiaji wa mashine za EFDs kwa wafanyabiashara, Mamlaka kuwatengenezea mazingira mazuri kwa walipa kodi, kudhibitiwa kwa eneo la forodha ambapo wajanja wachache walikuwa wanatumia mwanya huu kuikosesha serikali mapato” amesema Kidata.
Kwa mwezi Januari walikusanya Trilioni 1,079,993.20:
Katika  kipindi cha Januari pekee, Mmalaka hiyo ilikusanya  kiasi cha  Trilioni 1,079,993.20 kwa Tanzania bara na visiwani ambapo kiasi hicho ni sawa na asilimia 102 ya lengo la Sh Trilioni 1,059,864.00 kwa mwezi.
“Makusanyo  haya ya Januari yametokana na ari  na uthubutu ambao TRA imejiwekea katika kusimamia na kuhakikisha inaendelea kuziba mianya ya ukwepaji kodi na kuweka mazingira rafiki kwa mlipakodi  kwa kulipa kwa wakati na urahisi kwa kutumia mifumo mbalimbali iliyopo”ameongeza.
Faini ya mashine za EFDs kwa Wafanyabaishara:
Kidata amesema katika kipindi cha mwezi Februari pekee, Mamlaka hiyo imefanikiwa kukusanya  faini ya Sh 800milioni kwa watu wa jiji la Dar es Salaam ambapo walikiuka na kufanya makosa katika utumiaji wa  mashine za EFDs.
“Kuanzia mwezi Machi mwaka huu kila mtu anayetakiwa kutumia mashine za EFDs atumie  vinginevyo hatua kali za kisheria zitafuatwa”amesema Kidata.
Amesema utaratibu wa matumizi ya EFDs ulifanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza iliwahusisha  wafanyabiashara ambao wamesajiliwa kutoa VAT na awamu ya pili ilihusisha  wafanyabaishara ambao hawakusajiliwa na Vat ambao mauzo yao kwa mwaka ni zaidi ya Sh 14milioni.
Serikali kugawa bure mashine za EFDs:
Kwa upande wake Kamishna wa Kodi za Ndani kutoka TRA, Yusuph Salum alisema  serikali imeagiza Mamlaka ya Mapato nchini kutoa bure mashine za EFDs kwa wafanyabiashara  wadogo ambao uwezo wa kununua mashine hizo unaweza kuathiri mitaji yao ya biashara.
“Kwa sasa tuko katika hatua za mwisho kukamilisha manunuzi wa mashine za uniti 5700 na kwamba wafanyabiashara wakubwa hawatahusika na mgao wa mashine hizi za bure bali wao wataendelea na utaratibu wa zamani wa kujirejeshea gharama za mashine kupitia ritani za mwezi” amesema Salum.
Amesema pamoja na kuwepo kwa sheria inayomtaka mfanyabiashara kununua , kutumia mashine, kutoa risiti na kulipa kodi, TRA imebaini wafanyabiashara waliowengi hawana mashine hizo za kutolea risiti pindi wanapofaya  mauzona hivyo kuikosesha serikali.
Usajili wa magari:
Kidata alisema TRA, imefanya ukaguzi na kubaini kuwepo kwa magari ambayo yaliingizwa nchini na kusajiliwa bila kufuata taratibu za forodha hivyo kuyafanya yamilikiwe bila kulipiwa kodi stahiki na kwamba kuna jumla ya magari 9000 ambayo yanaingia nchini na kutolewa.
“Wamiliki wa magari wote  tayari  tumeshawataarifu  kufika TRA kufanyiwa uhakiki ili kuyalipia kodi stahiki lakini pia kumekuwa na matumizi mabaya ya misamaha iliyotolewa hasa kwa upande wa magari, hivyo utaratibu wa misamaha uliwekwa kwa ajili ya kuwapa nafuu wawekezaji ili wahusika wamekuwa wakiitumia vibaya kwani magari yameingizwa mengi kuliko mahitaji na kupelekea serikali kukosa mapato” amesema
Amesema sheria za kodi zinatoa misamaha mbalimbali kupitia utaratibu wa Kituo cha Uwekezaji cha Taifa(TIC) na mashirika yasiyo ya kiserikali na kwmaba nia na madhumuni ya misamaha hiyo ni kuvutia uwekezaji na kutoa unafuu wa huduma kwa jamii.
Kufutwa kwa bei elekezi:
Katika hatua nyingine,  Mamlaka hiyo imefuta bei elekezi katika  mchakato wa uthaminishaji wa bidhaa bandarini kwa sababu  ni kinyume cha sheria ya Jumuiay ya Afrika Mashariki na kwamba TRA itaendesha shughuli za kiforodha kulingana na sheria husika.
“Tumeona bei elekezi haisaidi kwa sababu uingizaji wa bidhaa unatawaliwa na sheria ya Afrika Mashariki ambapo na sisi Tanzania ni wanachama, hivyo Mamlaka itadhibiti ukaguzi na uthaminishaji halisi ili kila mfanyabaishara alipe ushuru na kodi kulingana na thamani ya bidhaa husika, hata hivyo uthaminishaji mizigo kwa wafanyabiashara umepelekea wengine kulipa kodi kubwa kuliko thamani ya bidhaa husika” amesema.
Leave A Reply