Nafasi za Kazi 15 Wizara ya Afya, Afisa Ustawi wa Jamiii Daraja La II
POST | AFISA USTAWI WA JAMII DARAJA LA II – 15 POST |
POST CATEGORY(S) | HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL HR & ADMINISTRATION RELIGIOUS STUDIES SOCIOLOGY, POLITICAL SCIENCE, COMMUNITY AND SOCIAL DEVELOPMENT TAXATION AND SOCIAL PROTECTION |
EMPLOYER | Ministry Of Health (MOH) |
APPLICATION TIMELINE: | 2022-05-05 2022-05-18 |
JOB SUMMARY | NA |
DUTIES AND RESPONSIBILITIES | i. Kuendesha Usaili wa wahudumiwa (watu wenye ulemavu, wazee, familia zenye matatizo, watoto na vijana wenye matatizo mbalimbali); ii. Kufanya ukaguzi wa mazingira wanayoishi wahudumiwa ili kupata taarifa zao kamili; iii. Kuandaa taarifa za usaili na ukaguzi wa mazingira ya wahudumiwa; iv. Kupokea na kukusanya taarifa za Ustawi wa Jamii kutoka kwa wadau na vituo mbalimbali vya Ustawi wa Jamii; v. Kupokea na kukusanya takwimu zinazohusu huduma za watu wenye ulemavu, wazee, malezi ya watoto na familia zenye matatizo; vi. Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya uandikishaji vituo vya kulelea watoto wadogo mchana, malezi ya kambo (foster care) na vituo vya walezi wa watoto wadogo mchana; vii. Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya msaada wa Rais kutoka kwa akina mama, waliojifungua watoto watatu au zaidi kwa mara moja; viii. Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya watoto yatima au wanaohitaji misaada mbalimbali; ix. Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi mbalimbali toka kwenye familia za watu wenye dhiki; x. Kuhoji na kuandaa taarifa za washitakiwa; xi. Kusimamia wahudumiwa katika makazi, vyuo vya mafunzo ya Ufundi Stadi vya watu wenye ulemavu, Mahabusu za watoto na shule za maadilisho; xii. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi |
QUALIFICATION AND EXPERIENCE | Kuajiriwa wenye Shahada ya Sanaa /Stashahada ya Juu katika fani za ‘Social Work’ , ‘Sociology’ ,’Psychology’,’Social Protection’,’Guidance and Counseling’,’Theology’,’Divinity’,’Child Protection’,’Social Policy’,’Early Childhood Development’ au ‘Social Gerontology’ kutoka Chuo cha elimu ya juu kinachotambuliwa na Serikali. |
REMUNERATION | TGS D |