WEMA SEPETU Alivyomrukia VAN VICKER Airport DAR- Video
MSANII mkubwa wa filamu nchini Ghana, Van Vicker, amewasili nchini Tanzania leo saa 10 alfajiri na kupokelewa na mwenyeji wake ambaye ni msanii wa Filamu Bongo, Wema Sepetu.
Van Vicker amekuja nchini kwa ajili ya kuzindua filamu yake aliyofanya na Wema inayoitwa ‘D.A.D’ inayotarajiwa kuzinduliwa Katika Ukumbi wa Mlimani City kesho Septemba 28 ambapo pia itakuwa ni siku ya kuzaliwa ya Wema Sepetu.
Comments are closed.