The House of Favourite Newspapers

Airtel Yanogesha Wiki ya Huduma kwa Wateja

Mkuu wa Kitengo cha huduma kwa wateja Airtel Bi Adriana Lyamba akimlisha keki mmoja kati ya wateja wa Airtel aliyetembelea duka la Airtel Morocco jijini Dar es Salaam, Bi. Pili Mgunda kwa niaba ya wateja ikiwa ni ahadi ya Airtel kuendelea kutoa huduma bora na zakibunifu. Airtel wiki hii ya huduma kwa wateja wamejipanga kuendelea kutoa huduma kwa ubunifu zaidi ili kuonesha thamani ya Mteja kupitia huduma zake zote.

 

AIRTEL yanogesha wiki ya huduma kwa wateja, yatangaza punguzo la simu za smartphone la hadi elfu 35 katika maduka yake.

 

Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel katika wiki hii ya huduma kwawateja imetangaza kuwa wataendelea na dhamira yake kuu ya kutoa huduma bora za kidigital huku wakisimamia kauli mbiu yao ya ‘Thamani ya mteja ni huduma’ kwa kushusha bei ya simu za Smartphone katika maduka yao yote nchini ndani ya wiki hii.

 

Mkuu wa kitengo cha huduma kwa Mteja Bi, Adrina Lyamba alisema “Airtel katika wiki hii ya huduma kwa wateja kama kawaida yetu tunaungana na watoa huduma wote katika shamra shamra za wiki yetu inayoanza tarehe 7 hadi tarehe 11 mwezi Oktoba na kuadhimishwa duniani kote.

Mmoja Kati ya Wateja wa Airtel aliyetembelea duka la Airtel Morocco jijini Dae Salaam, Bi. Pili Mgunda akimlisha keki Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja Airtel, Bi Adriana Lyamba ili kumshukuru kwa niaba ya wateja wengine kwa hudumia nzuri.

“Mwaka huu kauli mbiu ni ‘The Magic of Services’ kwetu inamaana kuwa ‘Thamani ya Mteja ni huduma bora’.

 

“Wiki hii tunawatangazia wateja wetu punguzo la simu za mkononi la hadi elfu thethini na tano (35,000) ili waendelee kufurahia kuwa ndani ya familia ya Airtel Mtandao bora wa Smartphone ‘The Smartphone Network’ alisema Bi. Lyamba.

 

“Yaani, Tunalenga kuendelea kuwapa wateja wote huduma bora zaidi na zinazotoa suluhisho la haraka kwa kila hitaji la mteja” Sisi Ni Mtandao Bora wa huduma za Smartphone’ alifafanua Lyamba.

Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja Airtel, Bi. Adriana Lyamba akishirikiana na baadhi ya wateja wa Airtel kukata keki leo ikiwa ni ishara ya kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoanza tarehe 7 hadi tarehe 11 mwezi Oktoba na kuadhimishwa duniani kote, “Mwaka huu kauli mbiu ya dunia ni ‘The Magic of Services’ ambapo kwa Airtel inamaana kuwa ‘Thamani ya Mteja ni huduma bora’

 

Bi Lyamba aliendelea kusema, “Katika kuadhimisha wiki hii, Airtel Tanzania tunatoa shukrani zetu kwa wateja wote wanaotumia huduma zetu, Pia tunawakaribisha katika maduka yetu ya huduma kwa wateja zikiwemo Airtel Money Branch zetu zote zaidi ya 1000 nchini ili kuendelea kujipatia huduma bora ikiwa ni pamoja na kusajili laini kwa mfumo wa alama za vidole (Biometria) au kupata huduma mbali mbali.”

 

Katika wiki hii Airtel itakuwa na matukio mengi maalumu kwa wateja lakini muhimu zaidi inawakaribisha wote katika ofisi za huduma kwa wateja ili kujipatia huduma bora kama vile kusajili laini mpya, kujipatia simu na vifaaa vya mawasiliano original kwa bei nafuu na kutakuwa na ofa kabambe maalum kwa ajili yako, ambapo puia Bi Lyamba alisema “watoa huduma wote wataeleza jinsi yakutumia huduma zote ikiwemo tuma pesa BURE na Airtel Money, Airtel Yatosha bando, huduma ya kukopa kwa Airtel Money yaani Timiza na nyinginezo nyingi.

Comments are closed.