The House of Favourite Newspapers

Aishi Manula Alikubali Bao Alilofungwa Na Morrison Taifa – Video

0

AISHI Manula mlinda mlango namba moja wa Simba amesema kuwa Bernard Morrison wa Yanga anastahili pongezi kwa kumtungua bao kwenye mchezo wa watani wa jadi uliochezwa Machi 8, Uwanja wa Taifa.

 

Morrison alifunga bao la ushindi dakika ya 44 kwa mpira wa adhabu akiwa nje ya 18 lilidumu mpaka mwisho wa kipindi na kuipa pointi tatu Yanga.

 

Manula amesema kuwa sheria zote alizofundishwa na makocha namna ya kupanga ukuta alizifuata mwisho wa siku akafungwa

“Kwa goli lile, golikipa unatakiwa kupiga makofi na kumpongeza mpigaji,” ,

Chanzo EFM

Leave A Reply