Takribani watu 18 wamepoteza maisha huku wengine kadhaa wakijeruhiwa baada ya treni ya abiria kugongana na basi huko Jakarta nchini Indonesia.
Dereva wa basi ni miongoni mwa watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi katika makutano ya barabara na reli huko magharibi mwa mji wa Jakarta.