The House of Favourite Newspapers

Ajibu Bado Anateswa na Goti

IMEFAHAMIKA kuwa mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu, huenda akaukosa mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya St Louis ya Shelisheli kutokana na majeraha ya goti ambalo pia linamsumbua Mrundi, Amissi Tambwe.

Mshambuliaji huyo, tayari amekosa michezo miwili; mmoja wa Kombe la FA timu hiyo ilipocheza dhidi ya Ihefu FC ya Mbeya na Ligi Kuu Bara waliocheza juzi Jumamosi dhidi ya Lipuli FC ya Iringa ambayo yote wal­ishinda.

 

Awali, kulikuwa na usiri mkubwa wa tatizo la mshambu­liaji huyo la kuto­cheza michezo hiyo miwili ya mfululizo, licha ya tetesi ku­wepo ana majeraha.

Ajibu kupitia ukurasa wake wa Instagram, jana alitupia picha akiwa maabara hospitalini akifanyiwa vipimo kwenye goti la kushoto.

 

Picha hiyo ilien­dana na maneno yake mazuri kwa aji­li ya kuwafahamisha mashabiki wa timu hiyo waliokuwa wakihoji sababu ya kutocheza michezo hiyo miwili.

Aliandika hivi akiambatanisha maneno yake na picha: “Habari zenu wapendwa, najua mlitamani sana niwepo kwenye ‘game’ yetu ya jana (juzi) ila hali halisi ndiyo hii.”

 

Kwa mujibu wa daktari mkuu wa timu hiyo, Edward Bavu, mshambuliaji huyo alipata majeraha hayo ya goti kwenye mechi ya ligi kuu dhidi ya Azam iliyomal­izika kwa Yanga kushinda mabao 2-1.

“Ajibu tulimbakisha Dar kwa ajili ya kufanyiwa vip­imo vya goti lake kabla ya kuanza matibabu, ni baada ya kuumia mechi na Azam.

“Hatima yake ya kucheza mechi ya kimataifa tutakayo­cheza Jumapili itajulikana baada ya kupata vipimo vya jeraha lake, hivyo tunaomba muda kidogo na taarifa zake zitatolewa,” alisema Bavu.

Wilbert Moland, Dar es Salaam

Comments are closed.