Labda ulikuwa ukilisikia lile vuguvugu la ugomvi mkubwa baina ya watu waliowahi kuwa wapenzi, Blac Chyna na mwanamuziki Ferrari. Ishu ni kwamba katika kipindi ambacho Chyna akiwa na Rob Kardashian, kumbe kisirisiri alikuwa akibanjuka na Ferrari kitu kilichomfanya mwanamuziki huyo kumpiga picha za utupu mwanamke huyo kisha kuachia picha moja tu huku akisema kwamba nyingine ambazo zitamuonyesha mwili mzima zitafuata.
Hali hiyo imemchanganya sana Chyna kiasi cha kuongea na mwanasheria wake, Lisa Bloom na kutoa uamuzi kwamba kama mwanaume huyo ataendelea kuweka picha za namna hiyo walizopiga chumbani basi atamfikisha mahakamani haraka iwezekanavyo.
Je, Ferrari atatulia baada ya mkwara huo au atajifanya kutokujali? Yetu macho.
Na: Nyemo Chilongani, GPL