Al Qaeda Yashambulia Burkina Faso
Mabomu yakilipuka kwenye hoteli ya Splendid mjini Ouagadougou.
Ouagadougou, Burkina Faso
Takriban mateka 30 wameokolewa baada ya wapiganaji kushambulia hoteli moja katika Mji Mkuu wa Ouagadougou nchini Burkina Faso na kusababisha mauaji ya takriban watu 20 na wengine 15 kujeruhiwa mapema leo Jumamosi.
Jengo la Hoteli ya Splendid
Watu kadhaa waliofunika nyuso zao walivamia hoteli hiyo ya Splendid na kuwateka watu kadhaa baada ya bomu kulipuka nje ya hoteli hiyo, kulingana na taarifa kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo.
Waziri wa Mawasiliano wa Burkina Faso, Remis Danjinou alituma ujumbe katika mtandao wa tweeter akisema takriban watu 30 wameachiliwa huru na kwamba oparesheni ya kijeshi kukabiliana na wapiganaji hao imeanza.
Polisi wakipambana na wapiganaji.
Amesema kuwa waziri wa nguvu kazi Clement Sawadogo ni miongoni mwa waliookolewa.
Hali ilivyokuwa.
]Tayari takriban watu 30 wamepelekwa hosptalini wakiendelea kupata matibabu aliongezea.
Haijajulikana iwapo kuna mateka ambao bado wamesalia katika hoteli hiyo, lakini mashahidi wameripoti milio mikali ya risasi katika ghorofa za juu mapema asubuhi.
Vikosi maalum vya Ufaransa pamoja na wanajeshi wa Burkinabe walihusishwa katika kuwaokoa mateka hao katika hoteli hiyo inayotumiwa na Umoja wa Mataifa pamoja na raia wengine wa Magharibi, alisema bwana Dandinou
Amesema kuwa idadi ya watu waliopoteza maisha yao haijulikani.
Waliojeruhiwa.
Afisa mkuu wa Hospitali Robert Sangare aliwanukuu baadhi ya manusura wakisema takriban watu 20 walifariki katika shambulio la kwanza, kabla ya vikosi vya usalama kuanza makabiliano na wapiganaji hao.
Baadaye, Waziri wa Mambo ya ndani wa nchi hiyo, Simon Compaore alisema kuwa miili 10 imepatikana karibu na mgahawa mwengine wa Cappucino ambao pia ulishambuliwa na wapiganaji hao.
Kundi moja linalofuatilia mitandao ya wapiganaji wa Jihad limesema kuwa wapiganaji wa al-Qaeda katika eneo la Maghreb wamekiri kutekeleza shambulizi hilo.Raia wa Ufaransa Leila Alaoui, ni mmoja kati ya waliojeruhiwa.