The House of Favourite Newspapers

Aliyemuua Mkewe na Kumficha Mbuyuni… Undani ni Huu!

UNDANI wa mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina Bernard Shumba mkazi wa Singida kugundulika na jeshi la polisi mkoani humo kuwa amemuua mke wake miaka minane iliyopita kisha kuufi cha mwili wa marehemu kwenye mbuyu, umeanikwa.

 

Habari kutoka chanzo cha kuaminika zinasema Shumba alikuwa mara kwa mara akiwa kwenye vilabu alikuwa akigombana na mtu anasema kwamba anaweza kumfanyizia kama alivyomfanya mkewe.

 

Kutokana na tambo zake hizo raia wema waliamua kuliarifu jeshi la polisi ambalo kwa weledi mkubwa walithibitisha kile alichokuwa akisema Shumba kwani alikwenda kuwaonesha polisi alikomfi cha  mkewe miaka minane iliyopita baada ya kumuua.

“Tuwapongeze polisi kwa kazi nzuri kwa sababu tambo za huyu bwana zimezaa matunda na kuonesha yalipo mabaki ya mkewe,” alisema mtoa taarifa wetu ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.“Nitoe wito kwa wananchi kwamba, watu wabaya wasifi chiwe siri kama bwana,” alisema.

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Deborah Magiligimba, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa baada ya kukamatwa alikiri kutenda kosa hilo na kwenda kuonyesha mwili wa marehemu aliokuwa ameuhifadhi ndani ya mbuyu ambapo jeshi hilo kwa kushirikiana na wananchi limefanikiwa kupata mabaki yake.

“Inadaiwa kuwa mnamo Julai 10, 2010 katika Kijiji “Baada ya 17, 2018 ambapo taarifa zilipopatikana zikidai kuwa alimuua.“Baada ya mtuhumiwa kukamatwa na kuhojiwa alikiri kufanya kitendo hicho na kuonyesha sehemu alipoufi cha mwili huo Machi 18, mwaka huu majira ya saa 10:00 jioni, “ alisema kamanda huyo wa polisi.

Mkuu wa polisi kituo cha Mkalama na timu yake ya makachero walifi ka eneo la tukio na kufanikiwa kupata mabaki ya mifupa yakiwa ndani ya mti huo. Baadhi ya mifupa imechukuliwa kwa ajili ya kupelekwa kwa mkemia wa serikali na iliyobakia ndugu wamekabidhiwa kwa ajili ya mazishi.

STORI: MWANDISHI WETU,SINGIDA

Comments are closed.