Amber Lulu hajawahi kuolewa jamani!
MWANADADA chakaramu kunako Bongo Fleva, Lulu Auggen ‘Amber Lulu’ ameruka mita mia moja kuwa hajawahi kuolewa bali watu wanamfananisha.
Amber Lulu ameliambia Gazeti la Ijumaa kuwa, kuna watu wanasambaza picha ikimuonesha akifunga ndoa, lakini ukweli ni kwamba siyo yeye, bali ni kufanana tu na huyo bibi harusi ambaye anaitwa Amber Rapa.
“Sijawahi kuonja ladha ya ndoa hivyo naomba watu wasinichurie. Huyo msichana anayesemekana ni mimi ni Amber Rapa na siyo mimi,” alisema Amber Lulu.
Stori: Imelda Mtema
Comments are closed.