The House of Favourite Newspapers

Anakunyima ‘chakula cha usiku’ bila sababu? SOMA HAPA!

IJUMAA nyingine imewadia, bila shaka msomaji wangu uko sawa kimwili na kiakili, kwa wewe ambaye mambo hayaendi sawa, nakuombea Mungu akufanyie wepesi. Mada yetu leo ni kama inavyojieleza! Yapo malalamiko mengi kutoka kwa wanaume ambao wapo kwenye ndoa halali au wapo kwenye uhusiano wa kudumu unaotambulika, kwamba wenzi wao wamekuwa wakiwanyima ‘chakula cha usiku’.

Hebu vuta picha, yaani umemuoa au unaishi naye, unampenda na yeye anakupenda, lakini inakatika hata miezi kadhaa, kila unapohitaji kuwa naye faragha, hataki! Mwingine atakwambia moja kwa moja, au mwingine atakuwa haishiwi visingizio ilimradi tu akukwepe.

Wengine wanafi kia hata hatua ya kuhama vyumba, baba analala chumbani mama analala chumba cha watoto. Kwa wale ambao wapo kwenye ndoa au uhusiano wa kudumu, watakubaliana na mimi kwamba hakuna kipindi kigumu kwenye uhusiano kama unapokumbana na changamoto ya namna hii. Kama bado hujawahi kukutana na hali hii, basi endelea kuwa makini na mwenzi wako kwa sababu itakapokutokea na ukawa hujui nini cha kufanya, unaweza kuhisi dunia nzima inakuelemea.

Unapotokewa na hali kama hii, unatakiwa kufanya nini? Kama wewe umeshawahi kutokewa, ulifanya nini mpaka mambo yakatulia na kurudi kwenye mstari? Ukweli wenye kuuma, ni kwamba wanandoa au wapenzi wengi wanapofi kia hatua hii, hushindwa kabisa kurekebisha mapenzi yao na hiyo inakuwa ni safari ya kutengana imeanza. Waulize watu wengi waliotengana au kupeana talaka, watakueleza wazi kwamba kipindi cha mwisho cha uhusianao wao, hawakuwa wakikutana kimwili.

Ni kwa kuzingatia umuhimu na unyeti wa suala hili, ndiyo maana nimeamua kuja na mada hii, tujadiliane na kujifunza nini cha kufanya inapotokea. TAFUTA CHANZO Wanawake watakuwa mashahidi wa hili kwamba haiwezekani tu mtu aamue kumkatalia mwenzi wake ‘kula tunda’ bila kuwa na sababu. Na unapoona tatizo linazidi kuwa kubwa,

kwamba muda unazidi kusonga mbele, lakini bado msimamo wake ni uleule, hapo ujue kuna tatizo kubwa ambalo ni lazima mlitafutie ufumbuzi. Wanawake wengi hutumia tendo la ndoa kama silaha yao ya mwisho, pale wanapoona kuna mambo hayaendi sawa na labda mhusika anaonesha kutojali.

Kwa hiyo unapoona mwenzi wako ameanza kukukwepa linapokuja suala la kukutana faragha, lazima utafute chanzo cha tatizo haraka. Mbinu nzuri ambayo wataalam wa uhusiano wanashauri itumike, huwa ni kujishusha kwa mwenzi wako na kutafuta muda mzuri wa kukaa naye na kumuuliza kwa upole, nini kimeukasirisha moyo wake au anasumbuliwa na nini mpaka ‘anakubania.

Kwa bahati mbayaa, wanaume wengi hufeli mtihani huu na matokeo yake, huendelea kufosi au wakati mwingine kutumia nguvu, kutumia maneno makali na kukataa kujishusha. Mapenzi ni hisia na ili hisia zipande lazima mwili na akili viwe na utayari. Ukimfosi unasababisha tatizo liwe kubwa, jishushe, zungumza naye kwa upole na utashangaa sababu atakazokueleza. Baada ya kuelewa

Anakunyima ‘chakula cha usiku’ bila sababu? tatizo, hata kama unajiona huna makosa, omba msamaha na mfanye ajione kwamba unamheshimu na kumjali, utashangaa mwenyewe akirudisha moyo wake nyuma na kukutimizia haja za mwili wako.

Hata hivyo, siyo wote wanaweza kukubali kukueleza tatizo ni nini! Yaani utajitahidi wee… utamtoa out! Mtaenda sehemu tulivu pamoja, lakini bado hatakwambia nini tatizo na mgomo utaendelea palepale! Inapotokea hali kama hii unatakiwa kufanya nini? Ni mambo gani yanayowafanya wanawake wafi kie hatua ya kugomea tendo? Usikose mwendelezo wiki ijayo!

Comments are closed.