Angalia Yanga na Simba Walivyomenyana Kiume Benjamini Mkapa
WATANI wa Jadi Yanga na Simba jana walimenyana vikali kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa jana Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar.
Kama kawaida ilivyodabi ya watani hao wa jadi ilikuwa upinzani mkali ulioanzia na mabishano ya mashabiki na kuendelea kwa wachezaji uwanjani.
Katika kipute hicho Yanga ndiyo walioanza kupata bao la penalti dakika ya 28 Tuisila Kisinda alipofanyiwa madhambi na beki wa Simba Joash Onyango.
Penalti hiyo ilipigwa na Michael Sarpong na kuingia wavuni.
Mambo yakizidi kutifuka uwanjani hapo Onyango ni kama alikuwa akitaka kufuta lawama ambaye ingemkabili kwa kusababisha penalti na kufunga bao la kichwa mpira uliopigwa na Luis Miquissone.