The House of Favourite Newspapers

Anitha Atengewa mil. 10 Acheze za Utupu

anita-2  MSANII kutoka kiwanda cha filamu Nollywood, Anitha Joseph ametengewa dau la Naira milioni 1.4 (milioni 10 za Kibongo) ili acheze filamu za utupu nchini Marekani.

Kwa mujibu wa Jarida la Vanguard, Anitha anayependa kupiga picha akiwa ‘ameyabusti’ matiti yake, alikuwa akichati na jamaa kutoka Marekani, Kane na kumng’ang’aniza kucheza filamu hizo za utupu zitakazokuwa zikimuingizia shilingi milioni 10 kila baada ya wiki tatu.

anita-1Licha ya kuwekewa dau hilo, Anitha hakuwa tayari kukubali zaidi ya kutoa matusi kwa Kane ambaye aliendelea kumshawishi kuwa, kuna mastaa kama yeye wa Nigeria wanacheza na kulipwa dau hilo nono huku wakiwa wamefunikwa nyuso zao.

Hata hivyo Kane hakuonesha kuchoka matusi na badala yake alimuandikia Anitha e-mail na kumtaka kama atakuwa tayari amtaarifu au atembelee mtandao wao.

 

Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam

Comments are closed.