The House of Favourite Newspapers

Asha Baraka awachamba Wakongo msibani

Mkurugenzi wa African Stars Entertainment (ASET), Asha Baraka amegeuka mwiba mkali kwa kuwachamba wanamuziki Raia wa DR Congo wanaofanya shughuli ya muziki nchini kwa tabia zao za kutohudhuria misiba ya wanamuziki wenzao wasio raia wa nchi yao.

 

Asha Baraka aliwachamba raia hao waliofurika Ukumbi wa Vijana uliopo Kinondoni jijini Dar, Jumatano iliyopita kwenye msiba wa mwenzao, Erick Cantona ‘Mugogo wa Mazizini Msanii wa Bei Kali’ aliyefariki Jumamosi iliyopita kwa ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar.

 

Mkurugenzi huyo aliwatolea mfano wa kifo cha mwanamuziki na kiongozi wa Bendi ya Vijana Jazz, Abdallah Mgonahazeru ambaye msiba huo walifurika wanamuziki na wasanii wa filamu lakini hakukuwa na mkongomani hata mmoja.

STORI: Richard Bukos

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO

Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.