Msemaji wa Simba Azikwa Magomeni Dar (Picha +Video)
MAREHEMU Asha Muhaji (50) aliyekuwa ambaye mhariri wa magazeti ya michezo ya Kampuni ya Habari Cooparation, Dimba na Bingwa, pia Afisa Habari wa Simba Sports Club ya Dar es Salaam, leo Alhamisi amezikwa kwenye makaburi ya Mwinyimkuu, Magomeni, Dar es Salaam.
Msiba ulifanyika nyumbani kwao Kijitonyama, Dar s Salaam, na kuhudhuriwa na wanahabari na wadau mbalimbali wa michezo ambapo makundi mbalimbali yalitoa salamu za rambirambi.
Miongoni mwa waliohudhuria msiba huo ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Wallace Karia na Katibu wake, Wilfred Kidao, Msemaji wa Simba SC, Haji Manara, Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, wachezaji na wadau mbalimbali.
Akimuelezea marehemu enzi za uhai wake msibani hapo kwa niaba ya Kampuni ya Habari Cooparation, Mohammed Mharizo alisema yeye ni miongoni mwa watu wengi waliofundishwa kazi na marehemu ambaye hakuwa mchoyo wa kuwarithisha wengine kipaji chake.
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS/GPL