The House of Favourite Newspapers

Askari 78 Waliofanya Vizuri Katika Kuzuia Vitendo Vya Uhalifu 2022 Wapewa yeVti vya Pongezi

0


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ACP. Muliro J. Muliro amewatunuku vyeti vya pongezi Askari Polisi 78 wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa utendaji kazi bora wa majumu yao katika kuzuia vitendo vya kihalifu kwa mwaka 2022.

Akiongea na waandishi wa habari leo tarehe 21 Januari 2023 katika hafla iliyofanyika Mesi ya maofisa wa Polisi Masaki, ACP. Muliro amesema kazi kubwa ya Askari Polisi ni kuzuia vitendo vya kihalifu, kwa mwaka 2022 Dar es Salaam kulikuwa na changamoto za vitendo vya kihalifu lakini askari na maofisa walifanya kazi kubwa na ya ziada ya kuzima fikra na mitazamo ya kihalifu katika
kuzuia vitendo vya kihalifu.


Kamanda Muliro amesema askari wote wamefanya vizuri, ila waliopewa zawadi ni wawakilishi kutoka kila eneo la utendaji kazi ambao wamefanya kazi vizuri zaidi kwa kujituma na kushirikiana na askari wenzao na wananchi katika kuhakikisha Dar es Salaam imekuwa salama kwa mwaka 2022
ACP. Muliro amebainisha vigezo vilivyotumia kuwapata askari hao ikiwa ni pamoja na nidhamu, weledi, uadilifu, ujasiri, kujituma, na utoaji huduma bora kwa wateja.

Leave A Reply