The House of Favourite Newspapers

Aunt na Kusah Wamnyima Usingizi Shamsa

0

KUNA kipindi waigizaji wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel na Shamsa Ford walikuwa kwenye bifu f’lani ambalo halikuwa na kichwa wala miguu, lakini sasa wapo sawa kabisa.

Hii ni baada ya Shamsa kueleza namna kapo ya Aunt na baby Daddy wake, Kusah inavyomnyima usingizi.

Ameposti picha yao na kuwaandikia; “Usidharau mapenzi ya mwenzio au kuona yule anakosea kuwa na yule. kila mmoja ana kitu chake anachokiangalia katika mapenzi kinachompa furaha.

“Kama mim ambavyo nafurahia na nazidi kufurahia kwa my forever man. Nimejikuta tu naipenda hii couple ipo kiuhalisia halafu vitabia vyao vinaendana hapo ukute anasemwa mtu…”

NA @SIFAELPAUL

Leave A Reply