The House of Favourite Newspapers

Azam FC Mzigoni Leo

0

KIKOSI cha AZAM FC leo Jumatano, Agosti 11, 2021, itakuwa na kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Big Bullets ya Malawi katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Kagame.

 

Ni majira ya saa 1:00 usiku, Uwanja wa Azam Complex mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kwa timu zote mbili kupambania nafasi ya kutinga hatua ya fainali.

 

Mshindi wa mchezo wa leo atakutana fainali na Express ambayo ilishinda nusu fainali ya kwanza Uwanja wa Azam Complex mbele ya KMKM kwa mabao 2-1.

 

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa wapo tayari kwa mchezo wa leo na wanahitaji ushindi ili kutinga hatua ya fainali.

Leave A Reply