The House of Favourite Newspapers

Azam FC Wapiga Hesabu Kali Kuimaliza Yanga SC

0

KOCHA Msaidizi wa Azam FC, Vivier Bahati amesema wamejipanga vizuri kuhakikisha wanashinda mchezo wao wa leo Jumapili dhidi ya Yanga ili kupunguza pengo la pointi zilizopo kati yao na kuzidi kujiweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara.

 

Azam, leo watakuwa wageni wa Yanga katika mchezo wa mzunguko wa pili wa ligi unaotarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam saa 2:15 usiku.

 

Azam itaingia katika mchezo huo ikiwa katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi na pointi 51 walizokusanya katika michezo 27 waliyocheza huku Yanga wao wakiwa na pointi 57 wakiwa nafasi ya pili katika msimamo.

Mchezo wa kwanza uliozikutanisha timu hizo katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam, Azam ilikubali kipigo cha bao 1-0 lililofungwa na Deus Kaseke Novemba 25, 2020.

 

Akizungumza na Championi Jumamosi, Bahati alisema: “Tunatambua kuwa ili kuweza kurudisha matumaini yetu ya kupambania ubingwa msimu huu ama kumaliza katika nafasi ya juu zaidi kwenye msimamo ni lazima tuhakikishe tunapata matokeo chanya dhidi ya Yanga kwenye mchezo wa Jumapili (kesho).

 

Kwa jumla asilimia kubwa ya wachezaji wako vizuri na wapo tayari kushindana ili kuweza kuhakikisha hatupotezi mchezo kwa mara ya pili mbele ya Yanga msimu huu na tutapambana kusaka ushindi.”

JOEL THOMAS,Dar es Salaam

Leave A Reply