The House of Favourite Newspapers

Azam Iko Fiti Kuelekea Ligi Kuu, Kimataifa

0

KOCHA mkuu wa Azam, George Lwandamina ameweka wazi kuwa maandalizi yao ya kabla ya msimu ‘Pre-season’
nchini Zambia, yamekuwa na
mafanikio makubwa katika kukiandaa kikosi chake kuelekea michezo yao ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Horseed ya Somalia.


Azam ipo Ndola, Zambia kwa
ajili ya maandalizi ya kabla ya msimu ya takribani wiki moja na nusu, ambapo wakiwa huko wamecheza michezo mitatu ya kirafiki dhidi ya Red Arrows, Kabwe Warriors na Zesco United uliochezwa jana Ijumaa.


Watakaporejea Azam watakuwa
kwenye maandalizi ya mwisho ya mchezo wao wa kwanza wa kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Horseed ya Somalia, unaotarajiwa kuchezwa Septemba 11 mwaka huu.

 

Akizungumza na Championi Jumamosi, Lwandamina alisema: “Tumekuwa na mafanikio makubwa kwenye kambi yetu ya muda hapa Zambia, ambapo tumefanikiwa kucheza michezo mitatu ya kirafiki, najivunia viwango vya wachezaji wangu na nina matumaini makubwa ya kufanya vizuri katika michezo miwili ya awali ya kombe la Shirikisho Afrika.”

 

Naye Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Azam, Zakaria Thabit ‘Zaka Zakazi’ alisema: “Kikosi chetu kinatarajiwa kurejea nchini Septemba 5, mwaka huu kwa ajili ya kufanya maandalizi ya mwisho ya mchezo dhidi ya Horseed ya Somalia ambao utafanyika Septemba 11, mwaka huu.”JOEL THOMAS,Dar es Salaam

Leave A Reply