The House of Favourite Newspapers

Azam Yaitambia Simba

KOCHA Mkuu wa Azam, Mrundi Etienne Ndayiragije amefunguka kuwa mchezo wao na Simba utakuwa na ushindani kwa kuwa sasa wote wanawakilisha nchi.

 

Azam itacheza mchezo dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ukiwa ni ule Azam yaitambia Simba Martha Mboma, Dar es Salaam wa Ngao ya Jamii.

 

Mrundi huyo alisema kuwa wamejipanga vizuri kuelekea kwenye mchezo huo na waamini kuwa watafanya vizuri.

 

“Tunaenda kukutana kwanza wote sasa hivi tumetoka kwenye mechi za kimataifa kila mmoja ana moto na mchezo utakuwa na ushindani mkubwa kati yetu ila nidhamu kwetu kama Azam tunatakiwa kuitanguliza mbele ilikuwa kwenye nafasi nzuri ya kupata matokeo,” alisema kocha huyo.

 

Ikumbukwe tangu msimu 2012/13 mpaka sasa, Azam FC imecheza mechi za Ngao ya Jamii zaidi ya mara tano na imetwaa taji hilo mara moja mbele ya Yanga kwa ushindi wa penalti

Comments are closed.