The House of Favourite Newspapers

Baada ya Kupigwa na Msauzi, Tony Ataja Dawa – Video

0

Bondia wa Mtanzania, Tony Rashid ameshindwa kuutetea mkanda wake wa Ubingwa wa ABU dhidi ya bondia Bongani Mahlangu raia wa Afrika Kusini katika pambano la raundi 12 lililopigwa usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.

 

Pambano la Tony na Msauzi huyo ni miongoni mwa mapambano yaliyowavutia watu wengi usiku wa jana ambapo tangu raundi ya kwanza Tony alikuwa akicheza vizuri na kumzidi mpinzani wake lakini cha kushangaza raundi ya 12, Tony akapigwa kwa TKO.

 

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa pambano hilo, Tony amesema Mahlangu alikuwa akitumia vitu vinavyodhaniwa kuwa ni dawa za kuongeza nguvu kinyume cha sheria za michezo jambo ambalo amesema tayari madaktari wamechukua sampuli ya vitu hivyo kwa ajili ya kwenda kuvipima.

 

“Mimi mwenyewe ninashangaa imekuwaje, kwa sababu tangu raundi ya kwanza mpaka ya 12 nilikuwa nampiga, nyote mmeona, lakini kuna kitu kilibadilika ghafla. Uongozi wangu walianza kushtuka tangu mapema kwenye kona yake alikuwa akipewa vitu kama dawa na kutumia, mimi sikujua.

 

“Zile ni dawa za kuongeza nguvu, haturuhusiwi kutumia dawa za kuongeza nguvu. Lakini tayari tumeshaliwasilisha kwa wahusika na madaktari wamevichukua vile vitu kwa ajili ya vipimo, endapo itabainika alikuwa akitumia dawa basi atanyang’anywa mkanda huo na kuvuliwa ubingwa. Tusubiri majibu tuone.,” amesema Tony.

 

Leave A Reply