The House of Favourite Newspapers

Babu Seya, Papii Kocha Waachiwa Huru kwa Msamaha wa JPM (Video)

Babu Seya na Papii kocha wakiwa na askari.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, ametangaza msamaha kwa Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na mwanaye Jonson Nguza (Papii Kocha) ambao waliofungwa maisha katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam na kutaka waachiwe huru mara moja kutoka gerezani.

 

“Tanzania tuna jumla ya wafungwa 39,000 ambapo wanaume ni 37,000 na wanawake 2,000.  Wafungwa waliohukumiwa wako 522 kati yao wanaume ni 503 na wanawake ni 19. Nimeamua kusamehe wafungwa 8157, ambapo baada ya msamaha huu wafungwa 1828 watatoka leo.

 

“Mfano wa watu niliowasamehe ni Mzee Mganga Matonya mwenye umri wa miaka 85 amekaa Gerezani miaka 37 na miaka 7 ya kukaa mahabusu. Nimeamua kusaheme familia ya Nguza Viking jina lingine anaitwa Babu Seya na Ndugu Johnson Nguza ama Papii Kocha.

 

“Nimeamua kuwasamehe wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa. Lakini katika kuchunguzwa kwingi wapo wafungwa ambao wametubu dhambi zao, wamekiri makosa yao kwelikweli,” alisema Magufuli.

 

Mwaka 2003, Babu Seya na wanaye watatu walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya kubaka na kulawiti watoto wa Shule ya Msingi Mashujaa, mwaka 2004, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar iliwahukumu wote wanne kifungo cha maisha jela.

 

Baada ya hukumu hiyo, walikata rufaa lakini mwaka 2005, Mahakama Kuu iliridhia hukumu hiyo ya kifungo cha maisha jela kwa wote wanne kabla ya Mahakama ya Rufaa kuwaachia huru Mbangu na Chichi Februari 2010.

VIDEO: JPM Amsamehe Babu Seya na Familia Yake, Sasa Wapo Huru

Comments are closed.