The House of Favourite Newspapers

Baby: Acheni kunichuria, sina mimba!

0

madahaNa Mwandishi wetu

Hivi karibuni zilivuja taarifa kuwa, msanii wa filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha ana kibendi ila kimeingia wakati hajajipanga hivyo anahaha kutaka kukichoropoa.

Chanzo makini kilicho karibu na staa huyo kilisema: “Huu ukimya wa Madaha ni kwa sababu amenasa mimba lakini inavyoonekana imeingia bila kutarajia, anachokifanya sasa ni kuangalia uwezekano wa kuichomoa.”

Baada ya kupata ubuyu huyo, mwandishi wetu alimtafuta msanii huyo ili kufungukia madai hayo ambapo alisema kuwa, asichuriwe kwani hana mimba ila watu wanasema hivyo kutokana na kushiba tu.

“Mtu akishiba tu, watu wanazusha una mimba, acheni kunichuria bwana, muda wa mimi kupata mimba bado na ikiingia siwezi kuitoa,” alisema Baby Madaha.

Leave A Reply