BABY J : NIKIIBUKA MAFICHONI, NITAWASHANGAZA WENGI !
MWANAMUZIKI anayefanya vizuri Bara na Visiwani kupitia Bongo Fleva, Jamila Abdallah ‘Baby J’ amesema kwa sasa yupo mafichoni lakini yuko mbioni kuibuka upya na atawashangaza wengi.
Akizungumza na Mikito Nusunusu, Baby J alisema kuwa ni kweli yuko kimya lakini kuna vitu anavipanga akimaliza ataibuka na kuwa vizuri kabisa.
“Najua watu wengi wanajiuliza nipo wapi lakini nashukuru sana Mungu nilipojificha ni kwa ajili ya mambo mazuri na si vinginevyo,” alisema Baby J.
Stori: Imelda Mtema
Comments are closed.