Baby Kidoti Aitwa Yahaya Mtandaoni
MWANADADA staa wa kuuza sura kwenye video za wasanii Bongo, ‘Baby Kidoti’, amepachikwa jina la Yahaya na mashabiki wa muziki huo baada ya kuona hajulikani anaishi wapi.
Awali Kidoti aliwahi kudaiwa kutokuwa na makazi maalum ya kuishi na badala yake kuishi kwa marafiki hapa Dar es Salaam.
Kidoti amepachikwa jina hilo baada ya kuweka video katika ukurasa wake wa Instagram ikimuonyesha akiwa hotelini bafuni.