The House of Favourite Newspapers

BAKULI HALICHAGUI MBOGA

NASHANGA bia yenyewe moja lakini asubuhi na wewe unakimbilia mchemsho wa nini? Paaaambeeee shoga, usione simba kaloa na mvua ukasema chui, inahu? Heheeeee heeeiyaaaaa! 

 

Shoga wanakwambia raha ya mwanaume awe na madeni na mwanamke sharti alijue jiko, upo nyonyo? Kama ulikuwa hujui jua sasa, hata kichungu nacho huonjwa ati, wareeeeereee!

Leo nipo na wale wanaoshangaa mtu kuolewa na mzee mzima, jamani kama wamekubaliana, wanapendana na kufikishana unataka akuoe wewe? Au akaoe mzee mwenzake? Haloooo eeeeehhhh ukiona kobe juu ya mti jua kapandishwa huyo! Shoga hata paka mzee naye hutamani maziwa, nashanga maneno yanakuwa mengi mwenzako akiolewa na mzee wee unanuna na kuweka majungu mtaani!

 

Siku zote nikisema kitu huwa namaanisha shoga yangu na usije kumtekenya hata siku moja aliyekubeba! Nina mashosti wangu wengi wameolewa na wazee siyo kwa sababu wamefuata pesa bali mapenzi ya dhati, kama wewe tu unavyompenda mwanaume mwenye rika sawa na wewe, upo? Sikwambii ukaolewe nao bali nataka na wewe uone kwamba wana haki ya kupenda na kuoa, siyo utasikia jitu linaanza; ‘ohhh ameshaponda raha zake ujanani anataka kumalizia kwa aliowazidi umri’, jamaaaani!

 

Labda nikupe siri shoga yangu, mara nyingi hawa wazee waliozidi umri wake zao huwa na busara katika maamuzi yao, yale mambo ya kupigwa pigwa mara kusimangwa na kusema ovyo walaaaa! Tena wakikutana na wanawake ambao wanajua maisha ni nini mbona wanadumu vizuri.

 

Waswahili wanasema bakuli hata siku moja huwa halichagui mboga na sifuri nayo ni namba japo inasahaulika, halooooo eeeeehhhh! Shangaa na kuongea mpaka mate ya kukauke wenzako wanaolewa na kwa taarifa yako wanadumu kuliko weweee unayekazana kusubiri kuolewa mpaka unafika miaka 45 ndiyo unashtuka.

 

Wale walioanzisha msemo wa umri si kitu katika mapenzi wala hawakukosea, wee endelea kuwa na akili za kenge anaikimbia mvua nchi kavu anaingia mtoni. Shoga sitaki niongee sana kwa leo naomba niishie hapa, ni mimi Anti Naa ukipenda niite Shangingi Mstaafu.

LOOH! Kumbe Desturi Za Wakurya Zinaruhusu Wanawake Kuoana

Comments are closed.