Khadija akizungumza na waandishi wa habari wa Global Publishers, leo.
Wewe ni mjasiriamali mdogo na una ndoto za kukua kibiashara na kupeleka bidhaa zako mpaka nje ya nchi? Basi habari njema ni kwamba, Balozi wa Good Will Foundation Ambassadors, Mtanzania Khadija Naif ametangaza fursa kwa wajasiriamali wadogo wa Kitanzania.
Akifafanua jambo.
Khadija ambaye alirejea nchini juzi akitokea Dubai alikotunukiwa heshima ya kuwa balozi wa WGFA kwa muda wa miaka miwili, alisema kwa kipindikirefu amekuwa akifanya kazi ya kuwasaidia Watanzania kujikwamua kiuchumi, kwa kuatafutia masoko nje ya nchi.
Akisikiliza maswali…
“Unajua kule Dubai na Falme za Kiarabu kwa jumla, bidhaa kutoka Tanzania zina soko kubwa sana, cha msingi ni Watanzania kuchangamkia fursa na kwa mfano, mimi mwenyewe huwa nachukua bidhaa kibao kutoka Tanzania, zikiwemo majani ya chai, kahawa, korosho na bidhaa zote za nafaka.
Akiwa makini kuandika maswali aliyokuwa akiulizwa
Akiwa na Kelvin Shayo wa Global TV
Akiwa na Laurance Kabende, Mhasibu Mkuu
Akiwa na Erick Evarist, mhariri wa Risasi Jumamosi
“Lengo langu ni kuwasaidia Watanzania ndiyo maana hata nimetunukiwa ubalozi wa heshima, nawaomba Watanzania wachangamkie fursa hii, ofisi zangu zipo Morocco na Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Na Kasmir Mseleche/ GPL
Comments are closed.