MARAIS wastaafu wawili wa Marekani, Bill Clinton, Barack Obama na Mbunge, Mazine Walters, ni miongoni mwa watu ambao wametumiwa mabomu ya siri kwenye vifurushi yaliyolenga kuwadhuru.
Kwa Waters, hii ni mara ya pili anatumiwa bomu la aina hiyo.
Hivi majuzi bomu liligunduliwa karibu na nyumbani kwa Bill na Hillary Clinton, na furushi jingine lililotiliwa mashaka lilitumwa kwenda nyumbani kwa Barack Obama, walisema polisi juzi.
Bomu jingine la aina hiyo lilitumwa kwa George Soros, tajiri na mtu maarufu kwa kutoa misaada ya kwa jamii ambaye pia ni mwanachama wa Democratic Party na mkosoaji mkubwa wa Rais Donald Trump.
Bomu lililotumwa nyumbani kwa Clinton lilikuwa limeandikwa jina la mkewe, Hillary. Serikali inachunguza video za kunasa matukio kujua furushi hilo lilifikishwa hapo kwa njia gani. Familia za Clinton na Soros zinaishi eneo la Westchester County.
Comments are closed.