BONIPHACE NGUMIJE | GAZETI LA RISASI JUMATANO, Toleo la Desemba 21, 2016
MSANII anaye-fanya vizuri katika Bongo Fleva, Baraka Andrew ‘Barakah The Prince’ amesema kupitia lebo yake ya Bana Music, ataha-kikisha anamrejesha kwenye kiwango chake, rapa Lord Eyes.
Akizungumza na safu hii, Barakah alisema Lord Eyes ni msanii mzuri aliyekosa usimamizi wa kazi zake, hivyo kupitia lebo yake anayoimiliki na mpenzi wake Najma, watafanikisha kupitia mipango yao.
“Lody Eyes anakwenda kurudi katika gemu kama zamani, lebo yangu imepania kumrudisha kwenye ‘peak’ tena na hata kuupeleka muziki wake kimataifa,” alisema Barakah. Bana Music pia inammiliki rapa Bonta aliyekuwa Weusi.
Comments are closed.