The House of Favourite Newspapers

BASHE Aliamsha Bungeni: Ushirika Huu Hauna Mtaji – Video

Mbunge wa jimbo la Nzega Mjini, Hussein Bashe, akichangia hoja katika bajeti ya Wizara ya Kilimo, amewataka wabunge kutoipitisha bajeti ya wizara hiyo ili Serikali ikaipitie tena na iwasilishe bajeti itakayoendana na mahitaji ya sekta hiyo.

Bashe ameyasema hayo Bungeni leo na kudai kuwa haiwezekani kilimo kinachoajiri zaidi ya asilimia 60 hadi 70 ya Watanzania ikatengewa asilimia 0.8 ya bajeti ya maendeleo ya Serikali kuu.

Comments are closed.