The House of Favourite Newspapers

Beki Simba SC Amtaja Kapombe

0

BEKI wa kulia wa Simba, Israel Mwenda, amesema amekuwa akipata msaada mkubwa kutoka kwa nahodha msaidizi wa kikosi hicho, Shomari Kapombe jambo ambalo limezidi kumuimarisha kila siku.

 

Mwenda amejiunga na Simba msimu huu akitokea KMC ambapo ndani ya kikosi hicho anagombea namba na Kapombe.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, Mwenda alifunguka kwamba: “Tangu nimejiunga Simba, Kapombe amekuwa msaada mkubwa kwangu, ni mchezaji mzoefu na ninajifunza mambo mengi kupitia yeye, amekuwa akinishauri vitu vingi kuanzia ndani na nje ya uwanja jambo ambalo limenifanya nizidi kuimarika kuanzia kwenye klabu yangu na hata timu ya taifa.”

HUSSEIN MSOLEKA

Leave A Reply