Ben Pol Atinga na Tausi Stejini Fiesta
Msanii wa Bongo Fleva, Ben Pol, ametinga stejini na msanii wa Bongo Movie, Tausi, akiwa kavaa shela katika Tamasha la Fiesta 2017 lililofanyika Leaders Club usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam. Wasanii hao waliwasisimua mashabiki kwa kuimba na kucheza kama mke na mme. Mashabiki waliwashangilia kwa staili walioibuka nayo.
(PICHA: MUSA MATEJA/GPL)