The House of Favourite Newspapers

NBC Yaendeleza Jitihada zake Katika Kusaidia Huduma za Jamii

Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati wa Benki ya NBC, Evance Luhimbo (katikati) akipokea cheti  kutoka kwa Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya Mshindano ya Gofu ya Hisani yaliyoandaliwa na Klabu ya Rotari ya Bahari, Hemaly Jethwa kwa kutambua udhamini wa benki hiyo. Kushoto ni Meneja Mahusiano wa NBC, Joseph Lema.
Picha mbalimbali za tukio la mashindano ya gofu ya hisani yaliyoandaliwa na Klabu ya Rotari ya Bahari na kudhaminiwa na          Benki ya NBC.
Mchezo wa Gofu ukiendelea kwa wachezaji.
Mashindano ya gofu ya hisani yaliyoandaliwa na Klabu ya Rotari ya Bahari na kudhaminiwa na          Benki ya NBC yakiendelea.
Wachezaki wakiendelea na mashindano hayo.
Mashindano ya gofu ya hisani yaliyoandaliwa na Klabu ya Rotari ya Bahari yakiendelea.
Hali halisi ya mchezo huo kama inavyoonekana.
Maofisa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), wakipiga picha. Walikuwa  wakitoa huduma za maji na kofia kwa wakimbiaji, washiriki pia walipata nafasi ya kujulishwa huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo na benki hiyo.

 

 

KATIKA kuendeleza jitihada zake za kurudisha sehemu ya faida yake kwa jamii, Benki ya NBC imedhamini hafla maalumu ya kuchangisha fedha  iliyoandaliwa  na Klabu ya Rotari ya Bahari jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

 

Hafla hiyo iliandaliwa na klabu hiyo ili kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia wenye mahitaji maalumu katika jamii ya watanzania ikiwemo mradi wa kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama, vyoo na ujenzi wa kituo cha kufundishia kwa njia ya mtandao katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja iliyopo eneo la Kunduchi jijini Dar es Salaam.

 

Akizungumza, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati wa NBC, Evance Luhimbo alisema NBC kwa miaka kadhaa imekuwa ikishughulisha katika kusaidia shughuli za jamii katika maeneo  mbalimbali kama vile elimu, afya na masuala ya ujasiriamali,

 

“Sisi ni jukumu letu kama benki kurudisha katika jamii sehemu ya faida tuipotayo katika biashara yetu, NBC ni benki kongwe yenye uzoefu katika kutoa huduma bora za kibenki kwa zaidi ya miaka 52, hivyo tutaendelea kusapoti miradi kama hii yenye kuleta tija katika jamii”, alisema.

 

Pamoja na hayo alisema mara baada ya kupokea maombi ya kuchangia hafla hiyo kutoka Klabu ya Rotari, benki yao haikusita kuitikia wito kwani ni imani jamii ikiwezeshwa kiuchumi na kielimu na jamii ikiwa na afya bora inaweza kuchangia vizuri katika kuleta maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

 

Aidha Bwana Lhimbo aliitaja baadhi ya shughuli za kijamii ambayo NBC imefaya ikiwa ni  pamoja na kutoa vifaa vya  ujenzi wa madarasa katika shule za mkoani Lindi, Zanzibar, msaada wa vifaa tiba katika Hospitali ya Rufaa Morogoro pamoja na kutoa elimu ya masuala ya kifedha na ujasiriamali katika shule mbalimbali nchini.

 

Baadhi ya miradi ambayo imeshafanikishwa na Klabu ya Rotari ya Bahari ni pamoja na matibabu ya moyo kwa watoto katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), ukarabati wa maktaba katika shule ya msingi buyuni, upanuzi wa kituo cha mafunzo ya ufundi stadi katika kituo cha masista cha Carmel, Kurasini, ukarabati wa maktaba katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja  pamoja na kutoa misaada ya aina tofauti katika vituo vingine vya walemavu na wasiojiweza.

Comments are closed.