BENKI ya NMB imewatangaza wateja watatu ambao wameibuka washindi katika droo ya mwisho ya kampeni ya matumizi ya ‘NMB Mastercard’ au ‘NMB Masterpass’ maarufu kwa jina la ‘MastaBata’.
Wateja hao watatu katika shindano hilo, Einstein Stephen Magebo, Simon Chacha, pamoja na Nuis Paul Kasambala wakiwa na wenza wao wanatarajia kusafirishwa na Benki ya NMB kwenda nchini Dubai kula Bata kwa siku nne mfululizo safari iliyogharamiwa na NMB kila kitu.
Akizungumza katika tukio hilo, Meneja Mwandamizi Huduma za Kadi wa Benki ya NMB, Bw. Stephen Jilala alisema washindi hao wamepatikana baada ya kuchezeshwa kwa droo ya mwisho ya Shindano la MastaBata lililoendeshwa kuhamasisha matumizi ya mfumo wa ‘NMB Mastercard’ au ‘NMB Masterpass’ kwa wateja wao.
Aliongeza kuwa mbali na washindi hao wateja kibao wa NMB waliotumia mfumo huo wa malipo pia wamejishindia shilingi 100,000/- kila mmoja na wengine wengi kujishindia simu janja za kisasa aina ya ‘Samsung S9+’.
Comments are closed.