The House of Favourite Newspapers

Bethidei ya Wema Kufuru!

0

Mkurugenzi  wa Endless Fame, Wema Sepetu akiwa amesimama mbele ya meza iliyokuwa imesheheni keki alizokuwa amendaliwa katika sherehe ya kuadhimisha   siku yake ya kuzaliwa iliyofanyikia ndani ya Ukumbi wa Wema Sepetu Hall, uliyopo ndani ya jengo jipya la Millenium Tower.

Meneja wa Wema (kushoto), Martin Kadinda, akimsaidia kukata moja ya  keki zilizokuwa zimeandaliwa muda mfupi kabla ya kuanza kuwalisha ndungu jamaa na marafiki zake.

Nelly Kamwelu (kulia), akipiga picha ya pamoja na Wema.

Wema akimlisha keki mpenzi wake Luis Manana.

Wema akikisiana na mpenzi wake huyo baada ya kulishana keki.

Weama akiwa amekumbatiana na mpenzi wake.

Wema akiwa amekumbatiana na mama yake mzazi.

Steve Nyerere akiongea jambo mbele ya Wema wakati wa kulishana keki.

Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika pozi na Wema.

Wema akifutwa kitu kwenye kidevu chake na mpenzi wake.

Msanii wa Bongo Fleva Ali Kiba (katikati), akitumbuiza kwenye Birthday hiyo.

Wema akiserebuka na dada zake kwenye hafla hiyo.

Martin Kadinda (kulia), akimkabidhi ramani ya kiwanja Wema.

Wema akifurahia jambo wakati akionyesha zawadi ya gari lake jipya.

Badhi ya waalikwa wakishuhudia gari la Wema.

Muonekano wa ndani wa gari jipya la Wema.

Wema akiwa ndani ya gari yake mpya.

MKURUGENZI wa Endless Fame Wema Sepetu, usiku wa kuamkia leo aliweza kufanya kufuru ya aina yake kwenye sherehe ya siku ya kuzaliwa kwake iliyofanyikia ndani ya Ukumbi wa Wema Sepetu Hall, uliyopo ndani ya jengo jipya la Millenium Tower, Kijitonyama jijini Dar.

Katika Sherehe hiyo iliyohudhuliwa na ndugu jamaa na marafiki zake ilifana kwa kiasi kikumbwa, ambapo Wema alipewa zawadi mbalimbali huku akionyesha zawadi yake ya gari jipya aina ya Range Rover  la mwaka huu.

Mbali na gari pia usiku huo meneja wake Martin  Kadinda aliweza kuonyesha baadhi ya bidhaa zenye nembo za Wema Sepetu ambazo zitakuwa zikiuzwa kwenye duka lake lililopo Mwenge TRA.

(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)

Leave A Reply