The House of Favourite Newspapers

Bila Messi Barcelona Yaipiga Juventus

0

BARCELONA ikiwa haina Lionel Messi jana usiku Agosti 8, walifanikiwa kuwapiga Juventus ya Cristiano Ronaldo kwa mabao 3-0  mchezo wa kuelekea msimu mpya kwa Barcelona mechi ambayo pia ilikuwa.

 

Magoli ya Barcelona yalipachikwa na  na mshambuliaji wao mpya Memphis Depay, Braithwaite na kinda  Puig.

 

Ushindi huu wa FC Barcelona umekuja muda sahihi na wakati sahihi kwani ilikuwa ni saa kadhaa baada ya Messi kuwaaga kwa machozi, lakini Barca wameonesha kuwa bado ni wapambanaji.

 

Kocha wa Juventus Max Allegri ameomba radhi baada ya kichapo hicho akisema kikosi chake kimefanya mazoezi kwa wiki moja hali iliyopelekea kichapo hicho.

 

“Naomba radhi kwa kupoteza mchezo lakini, tumefanya mazoezi wote pamoja kwa siku sita tu lakini pia Barca walikuwa kwenye ubora wao”.

Leave A Reply