The House of Favourite Newspapers

Bilionea Dangote akagua ujenzi wa kiwanda chake cha Saruji Mtwara‏

0

 Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (aliyesimama katikati), akizungumza na maofisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo y Nje, Viwanda na Biashara na Masoko, Kituo cha Uwekezaji Tanznia (TIC) na taasisi mbalimbali za serikali, walipokutana na Mtendaji huyo mkoani Mtwara jana kujadili kuhusu uzinduzi wa kiwanda hicho kikubwa cha simenti.

 
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (kushoto), akiwasikiliza kwa makini maofisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje, Viwanda, Biashara na Masoko na Kituo cha Uwekezaji Tanzani (TIC), waliotembelea kiwanda cha simenti cha Dangote kinachojengwa mkoani Mtwara jana kwa ajili ya maandalizi ya kuzindua rasmi Oktoba mwaka huu.
Mwekezaji kutoka Nigeria, Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (kushoto), akiwasikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Dangote Makao Makuu, Bw. Sada Ladan Baki (kulia), Mwakilishi Mkazi wa Makampuni hayo, Bi. Esther Baruti na Kaimu Balozi wa Nigeria, Bw. S. Umaru, alipokutana nao kwenye mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha simenti mkoani Mtwara jana.
 Bendera zikipepea kwenye kiwanda hicho kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki na Kati
Sehemu ya mitambo kiwanda hicho ambayo baadhi ujenzi wake umekamilika

 
Leave A Reply