The House of Favourite Newspapers

Bill Nas Alamba Dili la Mamilioni

Bill Nas.

MWANAMUZIKI ambaye alitamba kwenye gemu la muziki wa Bongo Fleva na ngoma ya Chafu Pozi, Bill Nas baada ya kula dili la Coce Studio Africa pamoja na kufanya matamasha mbalimbali, hivi karibuni amekula dili lingine la mtandao wa simu, ambalo amesema litampigisha hatua kubwa kwenye muziki wake.

Akichonga na ukurasa huu wa burudani, Bill Nas alisema kwamba, dili hilo ni la mkwanja mrefu na hivi karibuni atalifungukia moja kwa moja pale ambapo tangazo alilofanya litaachiwa na wenye nalo.

“Nimepiga dili ambalo nafikiri kwa mashabiki wangu litakuwa ni habari nzuri, sina uhuru wa kulizungumzia tu kwa sababu bado niliofanya nao hawajaliachia, lakini hivi karibuni wataliachia na nitakuwa wazi kusema ni milioni ngapi nimedaka,” alimaliza Bill Nas.

VIDEO: HIVI NDIVYO JOEL BENDERA ALIVYOFARIKI DUNIA!

Comments are closed.