The House of Favourite Newspapers

Binadamu wa Mwisho Kutembea Mwezini Gene Cernan Afariki Dunia

Astronaut Capt Gene Cernan speaks at the Omega Celebrates The 40th Anniversary of The Apollo Moon Landing at South Coast Plaza on July 11, 2009 in Costa Mesa, California. (Photo by Frazer Harrison/WireImage)

MAREKANI: Mwanaanga wa Marekani Gene Cernan, aliyekuwa binadamu wa mwisho kutembea kwenye Mwezi, amefariki dunia akiwa na miaka 82.

cernan_on_moon

Shirika la Anga za Juu la Marekani Nasa limesema limehuzunishwa sana kumpoteza mwanaanga huyo mstaafu.

Cernan alikuwa mmoja wa watu watatu pekee waliowahi kwenda Mwezini mara tatu na ndiye binadamu aliyetembea mwezini mara ya mwisho kabisa, mwaka 1972.

gene-cernan4

Maneno yake ya mwisho aliyoyasema kabla ya kuondoka kwenye Mwezi yalikuwa: “Tunaondoka jinsi tulivyokuja na, Mungu akitujalia, tutarejea na amani na matumaini kwa binadamu wote.”

Alikuwa kamanda wa chombo cha anga za juu cha Apollo 17 wakati huo.

Ni watu 12 pekee waliowahi kutembea kwenye Mwezi, na kati yao ni sita pekee ambao bado wako hai.

gene-cernan6

Bwana Cernan ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 82, siku zote aliwasisitiza vijana kufika mwezini ili wasimuache yeye pekee kubakia na sifa hiyo.

 

Comments are closed.