The House of Favourite Newspapers

Bocco: Tuna Kikosi Imara, Kitatupa Matokeo

0

JOHN Bocco, nahodha wa Simba amesema kuwa wana kikosi bora jambo ambalo linawafanya wawe na imani ya kupata matokeo mbele ya Kaizer Chiefs kwenye mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kuchezwa Mei 15.

 

Bocco alikuwa ni miongoni mwa wachezaji 24 ambao walikwea pipa jana kuelekea Afrika Kusini kwa kupita Kenya kwa Shirika la Ndenge la Kenya Airways aliliambia Championi Jumatano wana imani ya kufanya vizuri.

Ni Mei 15, Uwanja wa SA FNB Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes itakuwa na kazi ya kusaka pointi tatu kwenye robo fainali ya kwanza na ile ya pili itachezwa Mei 22, Uwanja wa Mkapa, Dar.

 

Bocco alisema: “Tuna kikosi imara kwa sasa na kila mchezaji anapenda kuona timu inapata matokeo hivyo tunawafuata wapinzani wetu tukiamini kwamba tunakwenda kusaka ushindi, mashabiki watuombee.

 

Malengo yetu kushinda ili tuweze kufikia malengo ambayo tulikuwa tumejiwekea tangu mwanzo wa msimu hilo linawekezana kwani wachezaji tumekuwa tukifuata yale maelekezo ambayo tunapewa na benchi la ufundi,”

Stori: Lunyamadzo Mlyuka, Dar es Salaam

Leave A Reply