Bodi ya Ligi Yasogeza Mbele Mechi Kariakoo Dabi Simba Dhidi ya Yanga
BODI ya ligi Kuu Tanzania TPLB, imetangaza mabadiliko ya tarehe ya michezo yote ya mzunguko wa 26 ligi kuu ya NBC ikiwemo mechi ya Dabi kubwa nchini kati ya vilabu vya Kariakoo Simba na Yanga.
Dabi hiyo sasa inatarajiwa kuchezwa Aprili 16, 2023 majira ya saa 11 jioni katika uwanja wa Benjamin Mkapa badala ya Aprili 9, 2023.
Mabalidiko ya mchezo namba 184 mzunguko wa 23 utakaozikutanisha Simba na Yanga yametokana na kutolewa taarifa ya kutoka kwa wamiliki wa Uwanja wa Mkapa ikitaja uwepo wa mkutano wa dini Aprili 9, 2023 siku ambayo ilipangwa kwa ajili ya mchezo huo.
Taarifa ya mabadiliko hayo ya tarehe yametangazwa rasmi na Bodi ya Ligi leo Januari 21, 2023.