
MWANAHARAKATI na mwandishi wa habari za Uchunguzi, Bollen Netti, aliyepotea Desemba 23 mwaka huu kwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana, amepatikana jana maeneo ya Tabata-Segerea jijini Dar es Salaam baada ya kuachiwa huru na watu hao.
Ngetti amekuwa akitekwa mara kwa mara kwa kipindi cha takriban miaka minne na kutekwa kwake siku hiyo kulikuwa ni mara ya nne.

