Bombadier 2 ‘Zaibwa’ Uwanja wa Ndege Lagos
NDEGE mbili aina ya Bombardier Dash 8 Q300 zilizokuwa zinamilikiwa na kampuni ya Topbrass Aviation Services Limited, zimedaiwa kuibwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Murtala Muhammed wa Lagos, Nigeria.
Ndege hizo zenye usajili wa 5N-TBB na 5N-TBC, ziko katikati ya mpambano wa kisheria kati ya mkodishaji, Seagold Investment Limited, na Topbrass Aviation Services.
Uchunguzi uliofanyika umeonyesha kwamba ndege hizo zimehamishwa mahali zilipokuwa zimeegeshwa katika uwanja huo na kupelekwa kwenye banda la kampuni ya Aero Contractors’ Maintenance and Overhaul (AMO) ambapo namba tayari zimefutwa na kwa sasa zikifanyiwa matengenezo ili ziondolewe Lagos na kupelekwa sehemu ambayo haijajulikana.
Sehemu ‘zilikofichwa’ ndege hizo.
Comments are closed.